Saturday 26 October 2013

Watoto Wetu Hadithi Ya Leo;Sungura na Mama mwenye shamba,Burudani- Kutoka kwa Mrisho Mpoto,Kwani ni Yeye MAMA!!

Watoto kipindi cha Baridi Kimeanza hapa tulipo.




Ni matumaini Yangu Watoto.Wazazi/Walezi Mnaendelea vyema kabisa na majukumu yenu..
Hapa tulipo Baridi imeanza..Basi watoto msisahau kuvaa nguo nzito/makoti,masweta  kwa kujilinda/kujikinga na baridi...
Pia shule zimefungwa kwa Wiki Moja..Basi Watoto Wangu wapendwa Muda huu muutumie Vizuri na kujifunza meengi  katika Jamii yanayo wajenga zaidi.Pia Wazazi/Walezi wenzangu huu muda mzuri sana kwa kuwafundisha  watoto ya kwetu..Kama kazi ndogondogo kulingana na umri wao,Nidhamu,Heshima na mengine meengi.

Watoto wa Afrika na Nchi nyingine vipi huko kwenu?
Jee Hadithi ya Leo mmejifunza nini?


  Shukrani;http://hadithihadithi.podomatic.com


Ni Mimi;Mama/Shangazi Yenu,Rachel[Kachiki]

Wednesday 23 October 2013

Watoto Na Lishe Bora;da'Sophi Kajembe wa Tupike Pamoja..!!!!!


Pureed vegetables Mahitaji: Carrot 1 Boga (350 gr.) Kitunguu 1/2 Viazi 2 Chumvi Mafuta ya olive (3 Tbsp.) Ingredients: 1 Carrot Pumpkin (350 gr.) 1/2 Onion 2 Potatoes Salt Olive oil (3 Tbsp.)

This is a video showing how to cook a puréed vegetables (a special meal for children from 18 months to 4 years old), for East-African users and all the swahili speakers all around the world. It's also subtituled in English. Please, subscribe to our channel if you like it. We are working to offer you more video-recipes in swahili, in our Youtube channel and in our web-site www.tupikepamoja.com

Tuesday 15 October 2013

Mahojiano na wadau wa darasa la Kiswahili Washington DC‏

Photo Credits: Panafricanvisions.com
Kiswahili inaaminika kuwa lugha asili ya Afrika inayozungumzwa na watu wengi kusini mwa jangwa la sahara.
Kama tunavyojua, ni lugha ya taifa kwa nchi za Tanzania naKenya, na pia yazungumzwa kwenye nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Burundi, Rwanda, Uganda na visiwa vya Comoro.
Ikizungumzwa na watu wanaokadiriwa kufikia milioni 100 hivi sasa, Kiswahili ndio lugha pekee ya kiAfrika iliyo miongoni mwa lugha rasmi za Umoja wa Afrika. Na inaaminika kuwa lugha ya saba kwa watumiaji wengi duniani
Na matumizi yake kama lugha inayozungumzwa na wengi wenye lugha tofauti katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati unaifanya lugha hii kuwa muhimu zaidi kwa watu wengi walio na mahusiano na / ama wanaotaka kujishughulisha na biashara, kazi ama diplomasia katika ukanda huo.
Kiswahili sasa kinafunzwa katika vyuo visivyopungua 50 hapa nchini Marekani, lakini pia inafundishwa kwenye vyuo vikuu mbalimbali Ulaya na hata bara Asia.
Kiswahili ni lugha muhimu katika habari, shule, kazi za kiofisi, kidiplomasia na hata usalama miongoni mwa mataifa na naamini ndio sababu hata jumuiya ya waTanzania hapa Washington DC wakaona ni jambo la busara kuanzisha darasa la kufunza Kiswahili kwa watoto hapa DMV.
Na leo, wawakilishi wa wahusika wa mpango huo, Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV (Washington DC, Maryland na Virginia) Idd Sandaly pamoja na walimu Asha Nyang'anyi na Bernadeta Kaiza wamekuwa wakarimu sana kujiunga nami katika studio za JAMII PRODUCTION hapa Washington DC.
KARIBU UUNGANE NASI
Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV (Washington DC, Maryland na Virginia) Iddi Sandaly akishiriki kipindi ndani ya studio za Jamii Production
Mmoja wa walimu wa darasa la Kiswahili hapa Washington DC Bernadeta Kaiza ndani ya studio za Jamii Production
Mmoja wa walimu wa darasa la Kiswahili hapa Washington DC Asha Nyang'anyi akishiriki kipindi ndani ya studio za Jamii Production
Twawapenda....Tukutane juma lijalo kwa kipindi kingine cha HUYU NA YULE tutakapohojiana na wadau wengine juu ya jambo jingine MUHIMU kwa jamii yetu
-- *JAMII PRODUCTION* "Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Saturday 12 October 2013

Watoto Wetu Katuni Ya Leo;Bongo Katuni-Kificho Animation!!!


Ni matumaini Yangu Watoto,Wazazi/Walezi wote Hamjambo na mnaendelea vyema.
Kwa  wale watoto wanaoishi Nga'mbo Mjiandae vyema na Baridi.
Na Wale Ndugu zetu Waislam tunawatakia Maandalizi mema ya Siku kuu  ya Eid.

Basi Nisiwachoshe,Leo nimewaletea Katuni[CARTOON].

Tuendelee....






Mmejifunza Nini Kupitia KATUNI[CARTOON]  Hii?
Shukrani;bongotoonz


Ni Mimi Mama/Shangazi Yenu Rachel [KACHIKI]

Dawati Ni Elimu Na Jerry Silaa!!!!


Jerry Silaa
Jerry Silaa;
 The "Dawati ni Elimu"” charity walk was be held on 12 October from Mnazi Mmoja to Bunge Primary School led by the first lady of United republic of Tanzania Mama Salma Kikwete. “The First of its kind mayoral ball aims to raise TZS 4.98 Billion towards providing 30,487 desks to primary and secondary schools in Ilala Municipality by end of financial year 2013/14. 100% of all funds shall proceeds towards realization of this project. Dawati Ni Elimu is a project by Hon Jerry Silaa, Mayor of Ilala Municipal council toward the build up of the annual Mayors ball. The Charity walk was sponsored by TSN Group, Eventlites, Continental Outdoor, A1outdoor and Vodacom and Managed by 361 degrees. ABOUT DAWATI Ni ELIMU. DAWATI Ni ELIMU is a project towards the Mayors ball that aims to solve the issue of shortage of desks in primary and secondary schools in Ilala municipality where by currently there is a lack of 30,487 desks. The project is an initiative under the office of the mayor of Ilala Municipal Council, this project seeks to raise a sum of 4.98 Billion Tanzanian shillings with the emphasis that the society can contribute and make change to solve the challenges by calling upon organisation and individuals to contribute to this noble cause.
See More;
 DAWATI NI ELIMU - charity walk 
Jerry Silaa;
;
DAWATI NI ELIMU;Kalisha mmoja Boresha Elimu!!!!!!

Wazazi/Walezi haya Tuungane Pamoja kusaidia watoto wetu wasikae Chini.

Shukrani;Jerry Silaa.

Saturday 5 October 2013

Watoto wetu ; Hadithi ya Leo-Nguruwe Watatu Wachanga!!!!




Natumaini Watoto,Wazazi/Walezi mnaendelea vyema.
Nini mmejifunza kupitia Hadithi hii?


Nawatakia Kila lililojema na mapumziko mema.

Shukrani;wambugu kamau

Ni Mimi Mama/Shangazi yenu;Rachel [KACHIKI]

Wednesday 2 October 2013

Watoto Na Maisha-Bethany Family children's home Tanzania!!!!!!

Wazazi/Walezi, Watoto..Leo "Watoto Na Maisha" Hawa ni Watoto wa Bethany Family Children's Home Tanzania...
Tukumbuke Leo tupo tuonaishi na Watoto wetu,Leo hii wapo wanaotamani kuishi na wazazi wao..Lakini kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao hawawezi/haiwezekani.....

Wapo wengine wanatamani/kuhitaji kuishi kwenye Vituo hivi..lakini wanashindwa/hawajui vipi watafika hapa..bado wapo Mitaani,Kula,Kulala,Kuvaa ni shida.

Mmhhh.. siwezi kuelezea zaidi/Nisikuchoshe..Endelea Kuangalia Maisha ya Watoto hawa..
Wengi wao wanaonekana Wenye furaha  na Amani.. na MUNGU azidi kuwa siamami..


Mzazi/Mlezi nini umejifunza kupitia Video hii?
Nini Msaada wako kwa Watoto wenye shida/kuhitaji?
Nini unaweza kuwaambia Watoto wako?


kwa Maelezo Zaidi ingia;http://www.bethanyfamily.net/