Thursday 20 June 2013

Watoto wetu na kujifunza yetu;da'Yasinta[KADALA] Anasema Mtoto umleavyo!!!!!!!!!!!!


KUJIFUNZA/KUJITEGEMEA MAISHA/KAZI ZA NYUMBANI!! AU MTOTO UMLEAVYO NDIVYO AKUAVYO!!



Tulipokuwa nyumbani mwezi wa sita mwishoni mpaka wa nane mwanzoni bahati nzuri ulikuwa ni msimu wa kuvuna. Tulimkuta Mzee ngonyani/babu amevuna mahindi. Na hapa mnamwona kijana Erik akimsaidia babu kupiga mahindi, kwa babu Songea Ruhuwiko.



Baada ya kazi nzito ya kupiga mahindi nguo zilikuwa zimechafuka kwa hiyo ni lazima kufua na hapa mnamwona anafua nguo zake....hapa ni Songea Ruhuwiko ....


Dada mtu naye siku yake ya dobi ikaja kama mnavyoona naye anafua nguo zake. Hii /hizi kazi ni moja ya kujifunza kuishi kwa kujitegemea.Uzuri wake maji tulikuwa nayo humu humu uani.


MAISHA NI KUJIFUNZA.
imeandikwa na da'yasinta [Kadala]wa;http://ruhuwiko.blogspot.co.uk/

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Hahahaha! Kachiki weweeeee mchokozi. .Lol..ahsante kiiibuoa hii tena. Samaki mkunje angali mbichi