Wednesday 27 November 2013

Ukatili Kwa Watoto;Mtoto wa Miaka 5 Acharangwa Mapanga.


Mtoto mwenye umri wa miaka mitano, Benson Nilah (pichani), amejeruhiwa vibaya kwa kucharangwa mapanga akituhumiwa kuchuma mapera bustanini kwa mtu katika kijiji cha Madizini Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma. Mtoto huyo alijeruhiwa vibaya sehemu za usoni na mdomoni na kusababishwa ashonwe nyuzi sita, alipatwa na mkasa huo mwishoni mwa wiki iliyopita na anayetuhumiwa kufanya kitendo hicho ni Ronginus Haule (58), mkazi wa eneo hilo.
kusoma zaidi »http://www.chingaone.com/

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Huu hakika ni unyama wa kutisha katika Songea yetu. Pole Benson.