Saturday 31 August 2013

Watoto Wetu;Hadithi ya Leo-Paka Wawili Wageuzwa Simba,Sehemu Ya-4-6!!!!!


Nimatumaini yangu Watoto Wangu Wazuri Hamjambo na Mnaendelea Vyema,Wengine mko kwenye maandalizi ya kurudi Shule,Wengine mmesharudi Shule.
Wazazi/Walezi nanyi nategemea mnaendelea vyema katika Malezi na Utafutaji.

Basi nisiwachoshe tuendelee na Hadithi yetu tuliyo ianza wiki iliyopita;Endela...







Jee mmejifunza nini kupitia Hadithi Hizi?
Nawatakia Mapumziko mema ya Mwisho wa Wiki.

Ni Mimi Shangazi/Mama Yenu Mpendwa;Rachel [KACHIKI]

Friday 23 August 2013

WatotoWetu;Hadithi ya Leo-Paka Wawili Wageuzwa Simba; Sehemu ya 1-3!!!!










Wazazi/Walezi na Watoto wangu Wazuri,Natumaini wote hamjambo na Mnaendele vyema na Masomo, Na wale waliokuwa kwenye Likizo ndiyo Inaishia sasa na Mnajiaanda kurudi Shuleni.

Hadithi  ya Leo,  Paka wawili wageuzwa simba ,
Shukrani;John Inniss

Mhhhhh Inatisha eehh..Haya Endelea kuangalia na itaendela...

Nawatakia mwisho mwema wa wiki,Na muwe watoto wasikivu na wenye kupendana.

Wenu;Shangazi/mama yenu;Rachel siwa[KACHIKI]

Asanteni Sana.


Saturday 17 August 2013

Watoto Wetu Leo;Hadithi ya Binti Chura,Sehemu Ya 1-2







Hadithi ya Binti Chura imepatikana toka katika Hadithi za Mama na Mwana Radio Tanzania. Kwa nakala ya hadithi hii na nyinginezo wasiliana na Radio Tanzania Dar es Salaam.
Tunaomba radhi kwa matatizo yoyote ya sauti katika hadithi hii


Watoto wazuri,Wazazi/Walezi, Nimatumaini yangu Mmefurahia sana Hadithi hizi...

Wazazi/Walezi/Watoto Wa zamani nini Maoni yenu katika vipindi vya sasa na vyazamani kwa Watoto?

Watoto;Nini mmejifunza kwenye Hadithi hizi?
Poleni watoto msiojua Kiswahili,Natumaini Wazazi/walezi watawasaidia Kuwatafsiria kwa Lugha mzijuazo.Pia natumai mtakuwa na hamu ya kujua Lugha hii ili msipitwe na Mambo mazuri/Kujifunza Meeengi ya Waswahili.

Niwatakie Mapumziko mema ya mwishoni mwa Wiki,Muwe Watoto wema na Watiifu kwa Wazazi/Walezi na Jamii pia.

Asanteni sana.
Shukrani;http://hadithihadithi.podomatic.com

Ni Mimi;Mama/Shangazi Yenu;Rachel siwa[KACHKI]

Friday 9 August 2013

Watoto Wetu Leo;Niwakumbushe Kipindi Cha MAMA na Mwana; Hadithi-siri ya Binti Mfalme;Sehemu ya 1-2.!!!!!!







Wapendwa watoto leo nawaletea Kipindi cha MAMA na Mwana. Wazazi/Walezi Leo nimewarudisha Nyuma/Zamani kidogo..Kuhusu MAMA na MWANA...Wengi wenu Mlikuwa/Tulikuwa wafuatiliaji wazuri sana..Enzi zetu na watangazaji wa RTD.Ninao wakumbuka..Shangzi/Mama;Sango Kipozi,Sarah Dumba,Debora Mwenda,Eda Sanga......Duhhh samahani kama nimekosea majina.
kulikuwa na Hadithi,Nyimbo,Vitendawili,Nyimbo,Kutembelea Mashuleni na Mambo Mengi..
Mhhhh  Unakumbuka Hii...Chei chei Shangazix2 Shangaziii shangazii...Uje Tena Shangazi x2 Tufurahi Shangazi Shangazii...

Jee wewe unamkumbuka nani na jee wewe ulikuwa Mpenzi wa kipindi Cha Watoto/Watoto Wetu/Chei Chei/MAMA NA MWANA?
Nini kingine ulichokuwa unakipenda kwenye kipi cha MAMA NA MWANA?
Hahahaha Tuma Salamu............

Nimatumaini Yangu Leo Mmefurahi sana.
Niwatakie JumaMosi Njema na Maendeleo mema ya EID.

Shukrani;http://hadithihadithi.podomatic.com/

Ni mimi Shangazi/Mama Yenu;Rachel [kachiki]

Wednesday 7 August 2013

Watoto na Michezo;Family Fun Day-Iliandaliwa na Hebron Church!!!!!!











Wazazi/Walezi na Watoto..Hii ilikuwa "Family Fun Day"..iliandaliwa na "Hebron Church"..Lakini haikuwa kwa Waumini/Washarika/Wakristo tuu..Japo waandaji ni Waumini/Waamini katika Kristo..Ilikuwa ya Watu wote,Ya wazi,Kwenye Viwanja[Park] kila mtu aliyependa kujumuika aliungana nasi/nao.
Ilikuwa ni  Kufurahi,Kucheza,Kula,Kujuana,Kujichnganya na Jamii..Pia kulikuwa na Kuchangia Watoto wenye shida..kama ulivyoona hapo juu kwenye Tangazo la[ZOE'S PLACE BABY HOSPICE] Na haikuwa lazima wewe kuchangia ndiyo ujumuike..kama uliguswa.. na kama siyo. Unaendelea Kujimwaga na Familia Yako.
Kulikuwa na Maswali mengi ya Watoto Wadadisi na kujifunza meengi....
Tulifurahi,Kujifunza,Kujuana,Kushirikiana Pamoja. kwani Mbele za MUNGU SOTE NI WAMOJA!!!

Wazazi/Walezi ni vyema tukajenga/kutenga nafasi ya kucheza pamoja na watoto wetu,wa Rafikiki zetu,Majirani na wengine.

 Asanteni sana na MUNGU azidi kutubariki soote...
Nkiripoti kutoka;STOKE GREEN[PARK],BINLEY ROAD.

Ni mimi;Mama/Shangazi Yenu,Rachel siwa[KACHIKI]